Image
Image

Kinana amjulia hali dereva wa gari lililoua viongozi wanne wa CCM Kilimanjaro.

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimjulia hali jana, Jackson Kimambo ambaye amelazwa katika hospitali ya KCMC Moshi mkoani Kilimanjaro baada ya kupata ajali wakati akiendesha gari kutoka kwenye Maadhimisho ya miaka 40 ya CCM mkoani humo, Jumapili, Feb 5, 2017. Katika ajali hiyo watu sita walikufa wakiwemo viongozi wanne wa CCM ambapo Kinana yupo mkoani hapa, kuongoza mazishi ya vingozi hao. Wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Sid Mecky Sadick.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akisaini kitabu ha wageni Ofisini kwa Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya KCMC ya Moshi, Kilimanjaro, Dk. Gileard Masenga (kulia), baada ya kumjulia hali dereva huyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya KCMC ya Moshi, Kilimanjaro, Dk. Gileard Masenga, akiwaaga Katibu Mkuu wa CCM Abdulraman Kinana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadick.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiagana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Said Mecky Sadick, baada ya zara hiyo ya kumjulia hali, dereva huo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment