Image
Image

Afya ya Mzindakaya ni njema, ataka taarifa za mitandaoni kupuuzwa.

Mwanachama na Kada mkongwe wa CCM Chrisant Mzindakaya akizungumza na waandishi wa habari kukanusha uvumi wa mitandao, katika  taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete jijini Dar es Salaam 13 Aprili 2017 (Picha na ITV).
Dar es Salaam
Kufuatia kusambaa kwa taarifa kupitia mitandaoni hivi leo zikidai kuwa Mwanachama na Kada mkongwe wa CCM Chrisant Mzindakaya amefariki dunia hatimaye taarifa hizo zimekanushwa na mwanasiasa huyo.
Mapema hivi leo Mwanasiasa huyo amezungumza na vyombo vya habari katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete nakusema kuwa yeye yupo imara kiafya hivyo wasambazaji wa taarifa hawana nia njema.
Mzindakaya ameongeza kwa kusema amesikitishwa mnoo na taarifa hizo ambazo zimezua taharuki na kuwaita wasambazaji wa taarifa hizo kuwa ni wapumbavu nakwamba muda wowote kuanzia sasa ataruhusiwa kuondoka hospitalini hapo.
"Madaktari wamenileza Afya yangu imeimarika mfano wa kijana wa miaka 20, hivyo ntaruhusiwa kutoka hospitalini hapa mda wowote.Amesema Mzindakaya.
Mwenyezimungu ampe umri mrefu zaidi Mwanasiasa huyu.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment