Image
Image

Wabunge waomba kuundwa kamati maalumu ya kupitia upya vitabu vyenye Makosa.

Baadhi ya Wabunge wameomba kuundwa kwa Kamati maalumu itakayopitia upya vitabu vyote vilivyosambazwa katika shule mbalimbali nchini  kuanzia darasa la Kwanza hadi kidato cha sita kufuatia kuwepo kwa makosa mengi kwenye vitabu hivyo.
Wabunge hao wametoa ombi hilo wakati wakichangia bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa Fedha wa 2017/2018, ambapo mjadala mkali umejitokeza  kuhusu uwepo wa vitabu vyenye makosa pamoja na wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito wakiwa shuleni.
Katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2017/2018, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inahitaji zaidi ya Shilingi Trilioni Moja Nukta Tatu kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake mbalimbali.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment