Image
Image

Darassa kufunga mwaka na mkwaju mpyaaaa...

Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Darassa amezungumzia ujio wake mpya.
Rapper huyo ambaye mara mwisho alisikika na ngoma ‘Hasara Roho’ ameiambia Dj Show ya Radio One yupo katika maandalizi ya kufanya hivyo ila kwa sasa asingependa kulizungumzia sana kwani yeye siku zote siyo muongeaji zaidi ya kazi.

“Kwenye single mpya watu wananijua mimi siyo mtu wa kuongea ongea kama sina kitu cha kuongea mara nyingi huwa nakuja kuongea nikiwa na kitu, kwa sasa naandaa project ambazo naamini nitakuja kufunga nazo mwaka watu wakae tayari tunakuja tuko poa kabisa” amesema Darassa.
Mwishoni mwa mwaka jana Darassa alifunga mwaka na ngoma Muziki ambayo alimshirikisha Ben Pol ambayo inatajwa kuwa ndio ngoma pekee kuwa hit ya kutisha kutoka kipindi hicho hadi mwaka huu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment