Image
Image

Aliyetekeleza shambulizi New York amefunguliwa Mashtaka.

Waendesha mashtaka mjini New York wamefungua mashtaka dhidi ya mhamiaji kutoka nchini Uzbek anayedaiwa kuhusika katika shambulio la gari dogo la mizigo lilitokea jana na kuua watu nane katika mji wa New York nchini Marekani.
Sayfullo Saipov anakabiliwa na mashtaka ya kuwasambazia vifaa kundi la kigaidi la Islamic State.
Waendesha mashtaka mjini New York wamefungua mashtaka dhidi ya mhamaji kutoka nchini Uzbestan anayedaiwa kuhusika katika shambulio la gari dogo la mizigo lilitokea jana na kuua watu nane katika mji wa New York nchini Marekani.
Sayfullo Saipov anakabiliwa na mashtaka ya kusaidia kutoa vifaa kwa kundi la kigaidi la Islamic State.
Akizungumzia mashataka yaliyofunguliwa kaimu mwanasheria mkuu JOON Kim amesema Saipov amefunguliwa mashitaka ya makosa mawili ya ugaidi.
Shitaka la kwanza ni kutoa vifa vya kusaidia maandalizi ya shambulio la kigaidi kwa kundi la IS, na shitaka la pili kusababisha uharibifu wa magari ambayo yalisabisha vifo na majeruhi.
Naye Rais Donald Trump akionekana na baraza lake katika ikulu ya white house, amesema kuwa anatarajia kuchukua hatua za haraka dhidi ya mfumo wa uhamiaji nchini humo.
Hata hivyo Rais Trump ametaka adhabu kali kutolewa dhidi ya watu wanaobainika kujihusisha katika vitendo vya kigaidi, kama hili la New York.
Awali Gavana wa New York, Andrew Cuomo, alimlaumu Rais Trump kwa madai kuwa anatumia tukio hilo kwa kujinufaisha kisiasa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment