Image
Image

WhatsApp yagoma kufanya kazi kwa nchi kadha ikiwemo Tanzania.

Mtandao wa kutuma mafaili mbalimbali kama Picha, Video na Sauti wa WhatsApp umekwama kufanya kazi kwa saa kadhaa kwenye baadhi ya nchi duniani ikiwemo Tanzania.
Ripoti zinasema tatizo hilo limeanzia nchini Uingereza kisha kuendelea katika nchi za Marekani, Italia, Ujerumani India na sasa nchi za Afrika Mashariki nazo zimepitia changamoto ya kukosa huduma ya mtandao huo.
Tatizo hilo limeelezwa kuanza majira ya saa mbili asubuhi ambapo maelfu ya watumiaji wa WhatsApp wameeleza kukosa huduma. Wengi wao wamelalamika kukwama kwenye baadhi ya majukumu yao kutokana na kutegemea mtandao huo kwaajili ya kuhamisha na kupokea mafaili yao.
Hadi sasa bado wamiliki wa mtandao huo ambao ni kampuni ya Facebook chini ya Mkurugenzi Mark Zuckerberg hawajatoa tamko juu ya tatizo hilo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment