Image
Image

MaiMai wasalimu amri, waweka silaha chini kurudi kwenye maisha ya kawaida.




Wapiganaji wa kundi la Maimai nchini Congo, wameitikia wito uliotolewa na rais wa nchi hiyo Felix Tshisekedi, wa kuweka chini silaha na kujiunga na jeshi la serikali au kurudi katika maisha ya kawaida.

Mamia ya wapiganaji hao kutoka kundi la UPCL wamejikusanya katika mji mdogo wa Kalunguta tayari kwa kusalimisha silaha zao.

Kulingana na meya wa mji wa Beni Bwanakawa Masumbuko Nyonyi aliyezungumza na BBC, hatua hiyo inatokana na wito wa rais wa taifa hilo Felix Tshisekedi wa kuwataka wapiganaji hao kuweka chini silaha mwezi wa Aprili mwaka huu.

Kulingana na meya huyo wito huo unatokana na mateso waliopitia wakaazi wa mji huo na viunga vyake mbali na mipango ya kuimarisha jeshi la taifa hilo ili kuweza kukabiliana na wapiganaji wa ADF ambao wametajwa kuwa maadui wakubwa wa serikali ya taifa hilo.

''Tangu rais wa DR Congo alipopita mjini Beni alitoa wito kwa wapiganaji wa Majimaji kuweka chini silaha kutokana na mateso walioyapitia wakaazi wa mji huo kufuatia uvamizi wa mara kwa mara wa wanamgambo wa ADF, baadhi yao wamekubali wito huo'', alisema.

Hatahivyo amesema kwamba ni kundi dogo la wapiganaji hao ambalo limekubali kuweka silaha chini ili kujumuishwa katika ujenzi wa taifa hilo ambalo baadhi ya maeneo yake yamekuwa yakikabiliwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi cha muda mrefu.

Huku akitoa wito kwa makundi mengine katika mji wa Beni kuiga mfano huo, Bwanakawa amesema kuwa baadhi ya wale waliokubali kuweka chini silaha watajumuishwa kwenye jeshi mbali na huduma nyengine za kitaifa huku wale wanaotaka kupelekwa nyumbani pia wakihudumiwa na kusafirishwa hadi makwao.

''Kila mtu ataulizwa aina ya kazi anayotaka kufanya au kujifunza iwapo ni ujasusi atapelekwa huko na kuna wale ambao watafunzwa kazi za mkono - kama huduma ya taifa. Kuna njia nyingi ambazo wakati watachukuliwa wataingizwa ili waridhike''.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment