Image
Image

EXCLUSIVE: TANZANIA KUPIGA HATUA KIUCHUMI

Wanafunzi Chuo kikuu UDSM wakimsikiliza bigwa wa uchumi kutoka nchini Idia.


Tanzania inaweza kupiga hatua za kimaendeleo na kiuchumi kwa kutumia rasilimali zake zilizopo nchini, ikiwa katika kupanua na kuwekeza  katika elimu ya juu ikiwemo ya biashara, na Kusimamia vyema wawekezaji katika sekta mbali mbali.

 Hayo yamebainishwa na Profesa Swami Partasaraty, bingwa wa kimataifa wa uchumi kutoka nchini india , alipo kuwa akitoa mhadhara kwa wanafunzi wa chuo kikuu cha biashara jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa nchi zinazofanikiwa ikiwamo india zimekuwa zikisimamia vyema sera za uwekezaji pamoja na kujikita katika utafiti ambao kwa kiasi kikubwa imeweza kusimamia uchumi wake bila kutegemea nchi wahisani.

Wanafunzi Chuo kikuu UDSM wakifuatilia kwa umakini somo linalotolewa na Mchumi wa dunia kutoka india - Chuoni hapo.
Hata hivyo kwa upande wake Mkuu wa chuo cha Biashara Chuo kikuu cha Dsm DR. ULINGETA MBAMBA, alisema kuwa kutokana na kukua
  kwa biashara na ongezeko la uzalishaji viwanda, hakuna budi kuweka mikakati katika kuwaandaa wanafunzi ktk kukabiliana na changamoto zinazojitokeza. 
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment