CHAMA cha
Wananchi (CUF), kimeionya Serikali kutotekeleza azma ya kuwakamata
viongozi wa chama hicho kwa kuwahusisha na vurugu zilizotokea mkoani
Mtwara hivi karibuni, kwa maelezo kuwa hatua hiyo, haitosaidia kumaliza
mgogoro huo.
Kauli hiyo ya CUF, ambayo imetolewa leo, jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, imekuja siku chache baada ya kutokea kwa vurugu mkoani Mtwara zilizotokana na shinikizo za wananchi kupinga uamuzi wa Serikali wa kusafirisha gesi kutoka mkoani humo.
Kauli hiyo ya CUF, ambayo imetolewa leo, jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba, imekuja siku chache baada ya kutokea kwa vurugu mkoani Mtwara zilizotokana na shinikizo za wananchi kupinga uamuzi wa Serikali wa kusafirisha gesi kutoka mkoani humo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Ibrahim Lipumba, akielezea jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam, na Kushoto ni Mwenyekiti wa Vijana CUF Taifa, Katani Katani. |
Kwa mujibu wa
Profesa Lipumba, CUF imepata taarifa kuwa Serikali imepanga njama za
kuwakamata wanasiasa mbalimbali wakiwamo viongozi wa chama hicho,
wakiwahusisha na vurugu hizo.
Alisema kuwa kitendo hicho, hakitokuwa sahihi kwa kuwa wanasiasa hawahusiki na vurugu hizo na kwamba hakitovumiliwa kamwe.
"Tumepata taarifa za kuaminika kuwa Serikali inapanga kukamata viongozi wa siasa wakiwamo wa CUF, kuwahusisha na yaliyotokea Mtwara, sisi kama CUF tunaimabia Serikali kuwa hilo si jambo sahihi na si kweli kama wanasiasa wanahusika, wasitafute mchawi katika hilo," alisema Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba, aliitaka Serikali kuruhusu wanasiasa kwenda mkoani Mtwara kwa kuwa siasa ndio jambo litakaloweza kusaidia kumaliza mvutano huo, baina ya Serikali na wananchi.
Alisema kitendo cha kuzuia kufanyika mikutano ya kisiasa hakitosaidia kumaliza mgogoro huo na kwamba nguvu ya siasa na ushawishi wa kisiasa unaweza kusaidia kumaliza mvutano huo.
"Wanasiasa wanahitajika Mtwara kufanya siasa, ili kumaliza kashikashi iliyopo mkoani humo, Serikali inatakiwa ikubali hilo na iruhusu tukafanye mikutano ya kuwaelimisha wananchi wa Mtwara," alisema Profesa Lipumba.
Mbali na hilo, Profesa Lipumba alilitaka Bunge kuunda kamati maalumu ya kufuatilia kwa kina sakata hilo, la gesi ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa jambo ilo.
Alilitaka Bunge pia kuhoji matumizi ya sh. milioni 540, ambazo katika bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012, ilitengwa kutekeleza mradi wa kufua umeme wa dharura kupitia eneo la Mnazi Bay, mkoani Lindi.
Profesa Lipumba alilaani matumizi ya nguvu katika kudhibiti vurugu hizo na kusema kuwa Serikali inapaswa kutafuta ufumbuzi wa chanzo cha vurugu hizo na si kushughulikia matokeo yake.
Alisema Serikali inapaswa kutekeleza miradi iliyoahidi kuitekeleza katika mkoa Mtwara, na kuacha maneno ya siasa bila vitendo na kupandikiza chuki kuwa watu wa Mtwara ni wachoyo wa rasilimali.
Aliongeza kuwa kutekelezwa kwa miradi hiyo ikiwamo ujenzi wa kiwanda cha Mbolea pamoja na vinginevyo, kutamaliza mvutano uliopo sasa.
Alisema kuwa kitendo hicho, hakitokuwa sahihi kwa kuwa wanasiasa hawahusiki na vurugu hizo na kwamba hakitovumiliwa kamwe.
"Tumepata taarifa za kuaminika kuwa Serikali inapanga kukamata viongozi wa siasa wakiwamo wa CUF, kuwahusisha na yaliyotokea Mtwara, sisi kama CUF tunaimabia Serikali kuwa hilo si jambo sahihi na si kweli kama wanasiasa wanahusika, wasitafute mchawi katika hilo," alisema Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba, aliitaka Serikali kuruhusu wanasiasa kwenda mkoani Mtwara kwa kuwa siasa ndio jambo litakaloweza kusaidia kumaliza mvutano huo, baina ya Serikali na wananchi.
Alisema kitendo cha kuzuia kufanyika mikutano ya kisiasa hakitosaidia kumaliza mgogoro huo na kwamba nguvu ya siasa na ushawishi wa kisiasa unaweza kusaidia kumaliza mvutano huo.
"Wanasiasa wanahitajika Mtwara kufanya siasa, ili kumaliza kashikashi iliyopo mkoani humo, Serikali inatakiwa ikubali hilo na iruhusu tukafanye mikutano ya kuwaelimisha wananchi wa Mtwara," alisema Profesa Lipumba.
Mbali na hilo, Profesa Lipumba alilitaka Bunge kuunda kamati maalumu ya kufuatilia kwa kina sakata hilo, la gesi ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa jambo ilo.
Alilitaka Bunge pia kuhoji matumizi ya sh. milioni 540, ambazo katika bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012, ilitengwa kutekeleza mradi wa kufua umeme wa dharura kupitia eneo la Mnazi Bay, mkoani Lindi.
Profesa Lipumba alilaani matumizi ya nguvu katika kudhibiti vurugu hizo na kusema kuwa Serikali inapaswa kutafuta ufumbuzi wa chanzo cha vurugu hizo na si kushughulikia matokeo yake.
Alisema Serikali inapaswa kutekeleza miradi iliyoahidi kuitekeleza katika mkoa Mtwara, na kuacha maneno ya siasa bila vitendo na kupandikiza chuki kuwa watu wa Mtwara ni wachoyo wa rasilimali.
Aliongeza kuwa kutekelezwa kwa miradi hiyo ikiwamo ujenzi wa kiwanda cha Mbolea pamoja na vinginevyo, kutamaliza mvutano uliopo sasa.
0 comments:
Post a Comment