Image
Image

EXCLUSIVE: BUNGE LATAKIWA KUHARAKISHA MUSWAADA WA SHERIA KWA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA.


Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limetakiwa  kuharakisha kupeleka Muswada wa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari bunge kusudi waandishi wa habari waweze kutekeleza  majukumu yao kwa kufuata kanuni na maadili  ya taaluma ya Habari.
 
Kauli hiyo imetolewa na Baadhi ya wabunge wakati wakichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na  Michezo kwa nyakati tofauti, ambapo wabunge hao wameiipongeza wizara hiyo kwa kuridhia Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari kwa kuwa itasaidia kukuza na kuiimarisha taaluma ya habari hapa nchini tanzania.
Mbunge wa viti Maalum (CCM) Esther Bulaya  alisema wakati umefika sasa  kwa waandishi wa habari nchini kuandika habari kwa kuzingatia maadili ya taaluma hiyo ikiwa ni pamoja na kuandika habari zilizofanyiwa utafiti wa kutosha na  wakina ili kutokuleta migogoro nchini.
Mhe. Bulaya  amewataka waandishi wa habari wasitumie vibaya uhuru wa habari walionao  kwa kutoa habari zinazoshabikia vyama vya siasa na zenye kuleta chuki na kupelekea malumbano miongoni mwa chama au jamii moja na nyingine na badala yake waandike habari zitakazo wafanya vijana waelewe nchi inakwenda wapi na sio habari zitakazo wafanya  vijana kujenga  visasi.
Kwa upande wake  mbunge wa Kondoa Kusini, Mhe. Juma Nkamia yeye alisema kupatikana kwa sheria ya kusimamia vyombo vya habari kutasaidia kuondokana na tatizo lililopo sasa la kuwa na waandishi wa habari wengi wasiokuwa na sifa maarufu kama ‘makanjanja’.  
Akizungumzia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Nkamia aliitaka serikali kupitia wizara ya habari kuhakikisha inafanya kila liwezekanalo kuyamalizia majengo yaliyopo Mikocheni ambayo yametelekezwa kwa muda mrefu. Aliongeza kuwa majengo hayo yaliwekwa jiwe la msingi na Rais wa awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi lakini mpaka sasa ni Serikali ya awamu ya nne na majengo hayo hayajakamilika.
Mhe. Nkamia pia aliitaka serikali kuiongezea bajeti TBC ili iweze kununua vifaa vipya na vya kisasa vya kurushia matangazo kwa kuwa vifaa vilivyopo vimechakaa. Aliongeza kuwa matangazo ya TBC hivi sasa hukatika katika kutokana na tatizo hilo.
Akiwasilisha hotuba ya Bajeti, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara aliliambia bunge kuwa serikali imeridhia kutungwa kwa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya habari na muswada wa kutunga sheria hiyo utawasilishwa bungeni hivi karibuni.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment