Image
Image

EXCLUSIVE: SERIKALI YATAKIWA KUACHA KUWA TEGENEZI KWA WAFADHILI, KUSUDI IWEZE KUTOKOMEZA MALARIA.

WATAALAMU wa afya wamesema Tanzania haitaweza kushinda vita dhidi ya vifo vinavyosababishwa na malaria endapo serikali haitaacha kuwategemea wafadhili.

 Akitoa mada juu ya ugonjwa wa malaria wakati wa kongamano la sayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili (MUHAS), Profesa Zul Premji, alisema Tanzania inahitaji kati ya dola milioni 300 za Marekani hadi 400, ili kupunguza vifo vinavyosababishwa na ugonjwa huo na kusikitika kuwa fedha za kupambana na ugonjwa mara zote zinatolewa na wafadhili badala ya serikali.
Watoto wakiwa ndani ya neti kujikinga na Mlaria
“Hii inaiweka vita dhidi ya malaria katika hatari kubwa endapo wafadhili wataamua kuacha kutoa fedha za msaada au kupunguza kiasi kinachotolewa. “Tanzania ina uwezo na vyanzo vya fedha vya kufadhili vita hii ya malaria, kama tukiamua kupanua vyanzo vya mapato ya kodi na kupigana na rushwa kikamilifu, tutafanikiwa,” alisema Premji.
Hata hivyo, alisema kuna haja ya kuanzisha mbinu nyingi zaidi za kupigana na malaria kuliko kutegemea matumizi ya vyandarua yenye dawa ambazo zimeonyesha kushindwa katika sehemu nyingi nchini ikiwepo Kanda ya Ziwa.
“Inatakiwa tuangalie ni jinsi gani tutajikinga na mbu si tu vyumbani lakini tukiangalia mbinu bora zaidi kama tunataka kushinda vita hii dhidi ya malaria.
“Tafiti zimeonyesha kuwa watu huumwa na mbu jike kabla hawajaenda kulala. Haitaleta maana kulala ndani ya vyandarua vyenye dawa kabla ya kuyamaliza mazalia ya mbu kwanza,” alisema.
Wakati huohuo, Tanzania imeshauriwa kutafuta mbinu za kuwawezesha vijana kiuchumi kama nchi ina lengo la kushinda vita dhidi ya VVU/ ukimwi.
Akitoa matokeo ya tafiti katika masuala ya VVU/ukimwi, Profesa Japhet Killeo alisema kampeni nyingi zimekuwa zikifanyika, lakini vijana wameshindwa kuendana na mbinu za kujikinga na ugonjwa huo ikiwepo matumizi ya kondomu kutokana na ugumu wa maisha.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment