Image
Image

WACHIMBAJI WADOGO KUNUFAIKA SASA.


Serikali imetenga  Sh.bilioni 9.8 kwa ajili ya mikopo ya vifaa kwawachimbaji wadogo nchi nzima ili kuboresha uchimbaji wao nawatakopeshwa kupitia vikundi watakavyojiunga na itakuwa mkopo endelevuili kuinua sekta hiyo ya madini kupitia wachimbaji hao.
Hayo yamezungumzwa  na Kamishna wa madini wa kanda ya kaskaziniEng.Benjamini Mchwampaka  wakati wa mahojiano na waaandishi wa habariyaliyofanyika katika ofisi za kanda hiyo zilizoko mkoani arusha.

Amesema kuwa kupitia mikopo hiyo itatoa fursa mbalimbali kwawachimbaji hao kupata vifaaa hivyo ili kuweza kuinua uchimbaji wao nakuwa wa kisasa zaidi ili kuongeza uzalishaji wa madini nchini ambapohivi sasa wamekuwa wakikwamishwa na ukosefu wa vifaa vya kisasa haliambayo wanachimba ila hawapati madini ya kutosha.
Ameongeza kuwa wachimbaji wadogo wa kanda ya kaskazini  badowanakabiliwa na changamoto mbalimbali  katika uzalishaji madiniikiwemo  kutokuwa na vifaa vya uchimbnaji vya kisasa ,bei kubwa yamilipuko na elimu ndogo ya uchimbaji madini hayo  hali ambayoinakwamisha jitihada zao za kuchimba madini hayo na kuwarudisha nyumakatika kujikwamua kiuchumiAlisema kuwa hivi sasa wachimbaji wadogo walio wengi wanachimba kwamazoea na vifaa duni ambapo elimu ya utambuzi madini  sehemu yalipo nindogo hali ambayo inasababisha kutopata madini yakutosha na kutumiagharama kubwa zaidi.
Eng.Mchwampaka alisema kuwa katika kanda hii wachimbaji wamekuwawakichimba kiholela bila lessen hali ambayo inaweza kuhatarishausalama wa maisha yao na hata kusababisha kifo na madhara mbalimbaliambapo  maeneo hayo yanachimbwa kwa kesi sana  hali ambayo ni hatarikwa  badala yake wachimbaji wafate taratibu za kuchimba eneo tengefukwa madini kwa maendeleo yao na usalama wa maisha yao kuepuka kupotezanguvu kazi ya taifa.Aidha aliongeza kuwa hivi sasa ofisi ya kanda imejiwekea mkakatimbalimbali ikiwemo kusogeza huduma karibu na wachimbaji katika kandahii hususan kutoa elimu ,ya uchimbaji wa madini kitaalamu zaidi,haliya masoko ,afya migodini  ,ajira na kutoa mafunzo kwa vitendo ya namnaya ulipuaji  mogodini sambamba na watatoa fursa ya namna ya uchimbajisalama na wenye tija na maendeleo kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

Eng.Mchwampakka alisema kuwa hivi sasa wako kwenye mchakato wa kuandaamaonyesho ya vito ,na madini mbalimbali  yatakayofanyika oktoba 28hadi 30 mwaka huu mkoani hapa  ambapo watahiusisha wafanyabiasharawote ncnini na nchi jirani ikiwemo Kenya ,DRC kongo ,Zambia ,Madagascar,Malawi ,Ethiopia ,Afrika ya kusini na Msumbiji ili kuwezakubadilishana uzoefu na kuweza kuongeza ushindani katika sekta yamadini nchini.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment