Image
Image

WAKAZI KIGAMBONI WAMUOMBA RAIS KIKWETE KUACHA KUWAAMINI WATENDAJI WAKE.


Wakazi wa Kigamboni wilayani Temeke wamemtaka Rais Jakaya Kikwete kuacha kuwaamini watendaji wake kuwa suala la wakazi la kupinga kuondoka katika eneo hilo kupisha ujenzi wa mji wa kibiashara limekwisha.

Wakizugumza kwa nyakati tofauti kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Kifurukwe kata ya Kibada jijini Dar es Salaam jana, wakazi hao zaidi ya 300 walisema kuwa hawako tayari kuondoka katika eneo hilo kwa gharama yeyote hata kama ni kumwaga damu wako tayari. 

Walisema suala hilo la kupisha ujenzi mpya wa jiji la kigamboni halijakwisha kutokana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi kuliendesha kinyume cha sheria na propaganda. 

Mwenyekiti wa Mkutano huo, Issaya Mathayo alisema wakazi hao hawana nia ya kumwaga damu ya mtu bali wanaitaka serikali kuwa makini ili kuepuka kuufikisha mgogoro huo katika hatua hiyo. 

“Mnajua suala la ardhi si la mchezo mchezo kuitoa ni rahisi lakini kuipata tena gharama yake ni kubwa hivyo tunaahidi hakuna atakaye ondolewa kirahisi pa ieleweke kuwa hatupingi maendeleo kikubwa sheria zitumike”alisema Mathayo. 

Alisema  sheria zikifuatwa wanaamini hukuna atakayeondolewa kwa kuwa kila ardhi inapobadilishiwa matumizi kwa ajili ya mandeleo, serikali hutumia  sheria zake za mipango miji kwa kuwapanga wananchi katika eneo husika na sikuwaondoa. “Kinachofanyika hapa ni ujanja hata hizo fomu ambazo tunaletewa tuzijaze zinaonekana si za kiserikali kwani hazina hata nembo ya taifa hali inayotutia mashaka”alisema Mathayo. 

Mathayo alisema kinachosikitisha hadi sasa hakuna mchakato wa kueleweka wa  tathimini za mali zao iliyofanyika kwa ajili ya fidia. 

Aidha, kuanzia jana wameamua kuicha kamati ilioundwa kwa ajili ya kusimamia maslahi yao kutokana na kamati hiyo kuwa upande mmoja na serikali.

Naye Mwalami Mwinyimvua, alisema mradi huo wananufananisha na ule wa makongo, kwamba ule mbona hauna manung’uniko ni kutokana na mradi huo kuendeshwa kwa kuzingatia sheria katika mali za wananchi husika.

 Alisema tangu kuanzishwa kwa mpango huo mwaka 2008 ieleweke kuwa hakuja kuwa na makubaliano yeyote kati ya serikali na wananchi hao kinachoendelea ni propaganda katika vyombo vya habari vya serikali. 

Mwinyi aliwalaumu madiwani wote wa Jimbo la kigamboni kushindwa kuwatetea wakazi hao katika kujua hatima yao na baadala yake wamejiingiza kwenye kazi ya udalali wa vinja kwa maslahi binafsi. 

“Sisi hapa tunaahidi hawa watu tumewachagua sisi katika nafasi hiyo lakini kutokana na upeo wao finyu wameamua kutuacha pekeetu watambue tutakutana nao mwaka 2015 hatuwezi kuwa na viongozi 
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment