Image
Image

EXCLUSIVE: SERIKALI YAWASILISHA RASMI LEO MUSWAADA WA MAREKEBISHO YA SHERIA YA FEDHA KWA MWAKA 2013 BUNGENI MJINI DODOMA.


Serikali leo imewasilisha bungeni Muswaada wa marekebisho ya sheria ya fedha kwa mwaka 2013 unaolenga kupunguza misamaha ya kodi kwa wawekezaji na hatimaye kurekebisha viwango vya kodi kwenye mishahara ya wafanyakazi.

Muswaada huo umewasilishwa punde tu na Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa wakati akisoma  Muswaada huo wa sheria ya fedha kwa mwaka 2013 katika kikao cha Bunge la Bajeti kwa mnwaka 2013/ 2014 Mjini Dodoma.

Mgimwa amesema kuwa marekebisho ya sheria hiyo yatasaidia Kurekebisha sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2011 ili kupunguza urasimu kwa ajili ya kuvutia wawekezaji kwenye miradi ya maendeleo inayolenga kuongeza mapato ya serikali na Kupunguza umasikini.
 Hata hivyo kwa mujibu wa waziri Mgimwa amesema chini ya muswaada huo sheria ya kodi ya mapato itafanyiwa marekebisho ili kuchochea ushiriki wa sekta Binafsi kwenye ujenzi wa uchumi wa Taifa pamoja na mambo mengine.

Aidha ameongeza kwa kusema kuwa muswaada huo lengo lake kuu unazitaka pia taasisi au mashirika yanayomilikiwa na serikali kuwasilisha asilimia 10 ya mapato ya mwaka kwenye mfuko mkuu wa serikali tofauti na sasa ambapo waziri mwenye mamlaka amepewa dhamana ya kuamua kiwango cha mchango wa taasisi hizo kwenye mfuko mkuu wa serikali.   

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment