Image
Image

IRAN YAZINDUA VIWANDA VYA KUSAFISHA MAFUTA


Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo amezindua Kiwanda cha Kusafisha Mafuta cha Lavan katika kisiwa cha Ghuba ya Uajemi cha Lavan.

Kufuatia uzinduzi huo, uwezo wa Iran wa kusafisha mafuta ya petroli kwa kiwango cha Euro-4 katika kiwanda hicho ni mapipa milioni 2,800,000.

Kiwanda hicho kilichoko kusini mwa Iran pia kina uwezo wa kuzalisha lita milioni moja za mafuta ya ndege kwa siku. 

Akizungumza katika uzinduzi huo, Rais Ahmadinejad amesema mradi huo ni muhimu sana kwa kuzingatia kuwa maadui waliiwekea Iran vikwazo hasa vya petroli iliyosafishwa ili kuzuia ustawi wa nchi hii. 

Ameongeza kuwa, sekta ya mafuta Iran ilikuwa tegemezi kwa usaidizi wa kigeni lakini nchi hii imeweza kujitegemea kikamilifu baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Kwa muda mrefu pamoja na kuwa Iran ni mzalishaji mkubwa wa mafuta ghafi ya petroli lakini ilikuwa ikinunua kutoka nje ya nchi petroli iliyosafishwa.

Hata hivyo kufuatia mashinikizo ya Marekani baadhi ya mashirika yaliacha kuiuzia Iran mafuta hayo.

Njama hizo za Marekani zimefeli baada ya Iran kufanikiwa kujitosheleza kikamilifu katika usafishaji wa mafuta ya petroli.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment