Image
Image

Ethiopia yapoteza asilimia 16.5 ya pato lake la kitaifa kutokana na utapiamlo


Taifa la Ethiopia linapoteza karibu asilimia 16.5 ya pato lake la kitaifa kutokana na athari za muda zinazotokana na utapiamlo miongoni mwa watoto kwa mujibu wa Shirika la mpango wa chakula duniani WFP.

Hii ni moja ya takwimu zinazoibuka kutokana na utafiti wenye kichwa "Gharama ya Njaaa barani Afrika" kuonyesha athari za utapiamlo kwenye mataifa 12 tofauti, huku taifa la Ethiopia likiwa la tatu matokeo yake kuchapishwa.
Kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita Ethiopia imepiga hatua muhimu katika kupunguza njaa na utapiamlo. 

Huduma za kutoa lishe zinazolenga akina mama na watoto na miradi mingine ya kuboresha kilimo vimeziacha familia nyingi na afya bora na katika hali nzuri ya kujilisha.

Hata hivyo, Shirika la WFP linasema kuwa athari zinazotokana na utapiamlo ni gharama kubwa kwa uchumi wa Ethiopia.

Ripoti hiyo inakadiria kuwa utapiamlo unaigharimu Ethiopia mabilioni ya dola kila mwaka.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment