Image
Image

RAIS WA MAREKANI BARACK OBAMA AANZA ZIARA YAKE YA NCHI TATU BARANI AFRIKA AMBAPO TANZANIA NI MIONGONI MWA NCHI HIZO.


Rais wa Marekani Barack Obama ameanza ziara yake barani Afrika ambapo anatarajiwa kuzuru nchi tatu.

Hata hivyo ziara hiyo imeghubikwa na wingu la mustakabali wa afya ya kiongozi wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela ambaye bado yuko hospitalini katika hali mbaya akihudumiwa na jopo la madaktari. Afrika kusini ni miongoni mwa nchi zitakazotembelewa na Rais Obama katika ziara hiyo ya wiki moja. Nchi nyingine ni  Senegal na  Tanzania.


Ikulu ya Marekani imesema itashauriana na familia ya Bwana Mandela kuona ikiwa Rais Obama anaweza kumtembelea mwanasiasa huyo mkongwe aliyelazwa katika hospitali ya mjini Pretoria kwa muda wa wiki tatu sasa.

Bwana Mandela na Obama hawajawahi kukutana ana kwa ana tangu Rais huyo wa Marekani alipochaguliwa kuingia madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2008.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment