Image
Image

EXCLUSIVE: MRADI WA BOMBA LA GESI ASILIA . WAZIRI MKUU WA TANZANIA MIZENGO PINDA AWATAKA WADAU MBALI MBALI NCHINI KUTOA ELIMU KWA WANANCHI ILI WAWEZE KUWA NA UELEWA NAO.


Mabomba ya mradi huo wa bomba  Gesi yakiwa Kwenye Gari.
Waziri mkuu Mizengo Pinda amewataka wadau mbalimbali nchini kuwa wajumbe wa kutoa elimu kwa wananchi ili kuwaongezea uelewa kuhusiana na mradi wa ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Mtwara na Songosongo hadi Dar es salaam na kutoa ushirikiano ili kuwezesha utekelezaji wa mradi huo wenye manufaa makubwa kwa taifa.
Mizengo Pinda - Waziri Mkuu Tanzania 
Shehena ya mabomba kwaajili ya ujenzi wa Bomba la gesi ukionekana hapo.

Waziri mkuu ameyasema hayo katika hafla ya kupokea shehena ya kwanza ya mabomba kwa ajili ya ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Mtwara na Songo Songo hadi Dar es salaam, ambapo amekumbushia madhumuni ya mradi huo kuwa ni kuongeza upatikanaji wa gesi asilia ili kuweza kuongeza uzalishaji wa umeme na matumizi mengine, ambapo alitolea mfano uzalishaji wa umeme kwa sasa aliosema zaidi ya nusu ya nishati hiyo inazalishwa kutokana na gesi asilia huku akisisitiza matumizi ya gesi asilia katika kufidia pengo la mahitaji ya umeme kufuatia mabadiliko ya tabia nchi.
Dk. Lu  YouQing, Balozi wa China - Tanzania

Yona Kilagane , Mkurugenzi Mtendaji - TPD.

Awali akimkaribisha waziri mkuu, waziri wa nishati na madini Profesa SOSPETER MUHONGO, amesema utekelezaji wa mradi huo utaleta manufaa kwa taifa ambapo juhudi za serikali zinalenga kukuza uchumi wa taifa kuendana na dira ya taifa ya maendeleo kufikia mwaka 2025, ambayo inalenga kuiwezesha nchi kuwa ya kiwango cha uchumi wa pato la kati.
Profesa Sospeter  Muhongo - Waziri wa nishati na madini  Tanzania.
Katika kufanikisha utekelezaji wa mradi huo kwa haraka, serikali imeamua kuupa kipaumbele kwa kuuingiza katika mpango wake wa matokeo makubwa ya haraka sasa (Big Results Now), ambapo ujenzi wake utachukua miezi kumi na minane na kukamilika mwaka 2014, ambapo utakuwa na uwezo wa kusafirisha futi za ujazo 784 kwa siku bila mgandamizo na ukiwekwa mgandamizo utasafirisha futi za ujazo 1002 kwa siku.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment