Image
Image

EXCLUSIVE: JWT LA THIBITISHA VIFO VYA WANAJESHI SABA WA TANZANIA WALIOFARIKI HUKO - DARFUR SUDAN


Esther Zelamula, Dar es salaam. 

Jeshi la Wananchi wa Tanzania - JWTZ limethibitisha kwamba, askari saba wa Tanzania wakiwemo sita wa jeshi hilo na mmoja wa Jeshi la Polisi Tanzania wameuawa kwa kupigwa risasi  jana na kikundi cha waasi wa Sudan katika eneo la Darfur nchini Sudan na askari wengine 14 wamejeruhiwa katika tukio hilo.

Akithibitisha tuki hilo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Kanali KAPAMBALA MGAWE amesema wanajeshi hao ni miongoni mwa walioko katika utekelezaji wa majukumu yao ya Umoja wa mataifa ya Kulinda amani nchini Sudan, ambapo kikundi hicho cha askari wa Tanzania kikiwa na afisa mmoja na maaskari 36  kilikuwa katika msafara wa kusindikiza waangalizi wa Amani kutoka Khor Abeche kuelekea Nyara eneo la Darfur, ambapo ghafla  kilishambuliwa na waasi hao umbali wa kilomita 20 kutoka makao makuu ya kikosi hicho.

Kanali Kapambala  Mgawe - Msemaji  wa JWT Tanzania.
Kanali Mgawe amesema tayari ujumbe maalum umeteuliwa kwenda Khartoum na Darfur kuzungumza na mamlaka kuhusiana na tukio hilo, ikiwa ni pamoja na kufanya mawasiliano kati ya JWTZ na Umoja wa Mataifa kuhusu uwezekano wa kuongeza uwezo wa kujilinda na mashambulizi inapobidi, pindi kikundi cha Tanzania kinapokabiliana na mashambulizi ya aina hiyo.

Akielezea hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na JWTZ baada ya askari wa Tanzania kushambuliwa katika tukio hilo na kutoa taarifa makao makuu ya Kikosi, Kanali Kapambala Mgawe anasema;

Akijibu swali la mwandishi wa habari aliyetaka kujua, ni namna gani ulinzi kwa askari wa Tanzania uliimarishwa hasa suala zima na magari wanayotumia wawapo katika majukumu yao ya kulinda amani, Kanali Mgawe alisema.

"Mazingira ya sasa yakule Dafur hapo katika hiyo chapter 7 ipo katika chapter 6 ambapo matumizi ya silaha yanakuwa relimited kwa sababu nikweli kama mnavyotambua ni muda mrefu tangu wamekwenda hawa askari na hapakuwahi kujitokeza hilo sasa Umoja wa mataifa unapo angalia hali hiyo baadae hua inabadilisha utaratibu na tunadhani tutashauriana nao ili waweze kubadilisha utaratibu ili tuwe katika Comfiguration nzuri zaidi yakuweza kupigana au kutumia nguvu ilikuweza kuokoa maisha ya watu" alisema Mgawe.    

Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ lilikuwa na askari 875 wa kulinda amani Darfur nchini Sudan.




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment