Image
Image

IRAN: YATOA WITO KWA MISRI.


    Washauriwa kuwa watulivu vuguvugu la misri.

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeelezea masikitiko yake kufuatia mauaji ya makumi ya watu katika machafuko ya hivi karibuni Misri na kutoa wito kwa pande zote hasimu nchini humo kujitadhidi kudumisha utulivu.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Abbas Araqchi ametoa kauli hiyo na kuongeza kuwa, Tehran ina matumaini kuwa watu wa Misri watakuwa waangalifu na kutumia hekima ili kuvunja njama za maadui wanaotaka kuvuruga mapinduzi yaliyojiri nchini humo mwaka 2011. 

Araqchi ametoa wito kwa vyama vya kisiasa na viongozi wa Misri kuheshimu mshikamano wa kitaifa, haki za kimsingi za wananchi na misingi ya demokrasia ili kufungua njia ya mazungumzo na maelewano ya kitaifa.

Wakati huo huo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amelaani vikali ongezeko la machafuko nchini Misri.

Amevitaka vikosi vya usalama vya nchi hiyo kuheshimu haki za binadamu kikamilifu katika vitendo vyao, zikiwemo haki za kujieleza na kujumuika. 

Ban ametaka tena Bwana Mohammed Morsi na viongozi wengine wa chama cha Muslim Brotherhood ambao sasa wapo kizuizini waachiliwe huru mara moja au kesi zao kuangaliwa kwa njia ya uwazi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment