Image
Image

POLISI NCHINI MAREKANI YAWATIA NGUVUNI WATU 150 WANAOJIHUSISHA NA VITENDO YA UBAKAJI NA UKAHABA DHIDI YA WATOTO.


Polisi nchini marekani ikiwa imemshikilia moja ya mtuhumiwa wa vitendo vya ubakaji na ukahaba nchini Humo.

Polisi nchini Marekani imewatia mbaroni watu 150 kwenye oparesheni ya kupambana na vitendo vya ukahaba na ubakaji dhidi ya watoto nchini humo.

Polisi huko nchini Marekani imeeleza kuwa, watu hao 150 walitiwa mbaroni katika miji 76 ya nchi hiyo kwa tuhuma za kuwanajisi na kuwabaka watoto. 

Oparesheni hiyo ilifanikiwa kuwakusanya watoto 105 waliokutwa kwenye vituo vya malori, hoteli mbalimbali, kumbi za starehe na kwenye makasino. 

Vitendo vya ubakaji na udhalilishaji wa kijinsia kwa watoto, ni moja kati ya jinai kubwa zinazofanywa nchini Marekani. Imeelezwa kuwa, kiwango kikubwa cha  watoto wenye umri wa miaka 13 hadi 16 huwa wahanga kwa kutumbukia kwenye  vitendo hivyo vilivyo kinyume cha maadili ya mwanadamu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment