Mwanamke
mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 hadi 30 amekutwa amekufa
katika makaburi ya Majengo soko la mjini Kahama mkoani Shinyanga huku mwili
wake ukiwa ametobolewa macho na kuonesha kupigwa na kitu kizito usoni.
Mwanamke huyo ambaye
hajatambulika jina lake na anakotoka alikuwa amevaa Blauzi nyeusi yenye madoa
meupe, viatu vyenye urembo wa silva, mnene kiasi, mweusi na mwenye nywele
ndefu.
Mwili wa Mwanamke
huyo amegunguliwa leo majira ya saa sita Mchana baada ya watu waliokuwa
wanachimba kaburi kuuona mwili huo pembeni ya eneo hilo na kutoa taarifa Polisi
.
Kwa mujibu wa
majirani wanaoishi eneo la makaburi hayo, tukio hilo linakisiwa kutokea usiku wa
kuamkia jana huku baadhi ya kina mama wakisema kuwa walisikia sauti ya mwanamke
akipiga mayowe katika eneo la mnadani
0 comments:
Post a Comment