Image
Image

MAN UNITED YATAJWA KUINGIA KWENYE VITA KALI YA KUMUWANIA BALE.



Mtandao wa Sky Sports umesema vyanzo vyake vya kuaminika vya habari vimeuambia mtandao huo kwamba Tottenham wanafikiria kukubali ofa kutoka kwa klabu kadhaa kwa ajili ya Gareth Bale - na kusisitiza kwamba bado hawajakubaliana na Real Madrid kumuuza winga huyo. 

Real wamekuwa wakiongoza mbio za kumsajili Bale wakati wa dirisha hili la usajili, lakini sasa kumetokea klabu nyingine ambayo inaipa upinzani katika kushinda mbio za kumsaini Bale.

Ripoti nchini Spain wikiendi hii zilikuwa zikisema kwamba Madrid walikuwa wanamalizia taratibu za mwisho za kumsaini Bale katika dili ambalo lingevunja rekodi ya dunia - huku Spurs wakiripotiwa kukubali kumuuza nyota huyo.

Japokuwa, sasa imefahamika hakuna makubaliano yaliyofikiwa baina ya Tottenham na Real na sasa klabu hiyo ya White Hart Lane inafikiria ofa za klabu nyingine.  

Manchester United wamekuwa wakitajwa kuvutiwa na Bale, lakini inabaki kusubiriwa kama David Moyes ndio kocha mwingine aliyejiingiza katika mbio za kumtaka winga huyo mwenye miaka  24.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment