Image
Image

POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM YASEMA: UCHUNGUZI WA KIFAA KILICHOONEKANA NA KUIBUA HOFU KWENYE ENEO LA KANISA LA KKKT USHARIKA WA KIJITONYAMA WABAINI KUWA SI BOMU.

Jeshi la polisi kanda maalum limetoa ufafanuzi kuhusu kifaa kilichodhaniwa kuwa ni Bomu kilichoonekana katika eneo la kanisa la kkkt usharika wa kijitonyama jijini dsm jana ambapo limesema baada ya uchunguzi imegundulika kuwa ni kifaa cha kunasia sauti anga za juu kinachotumiwa na mamlaka ya hali ya hewa.

Akizungumza na waandishi wa habari huku akiwa na mataalamu kutoka mamlaka ya hali ya hewa Kamanda wa kanda maalum Kamishna wa Polisi Suleiman Kova amesema kifaa hicho kinachojulikana kama radio sonde huwa kinarushwa kila siku huku kikiwa kimefungwa puto (baloon) na baada ya kuruka umbali wa kilometa elfu ishirini balooni hupasuka na kifaa hicho kurudi ardhini .

Akizungumzia matukio ya uhalifu kamanda Kova amesema jumla ya watuhumiwa 136 wamekamatwa kati yao majambazi hatari wanne wakiwa na bastola mbili pamoja na risasi 36,ambapo pia jeshi hilo linaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio la bomu la kienyeji lililorushwa katika kanisa la kkkt tabata pamoja uchunguzi dhidi ya watumishi bandia wa vyombo vya dola waliokamatwa hivi karibuni.

Wakati huo huo kampuni ya simu ya mkononi ya vodacom imaenzisha utaratibu maalum wa m-pesa utakaotumiwa na makampuni makubwa ili kulipa mishahara kuepuka vitendo vya uporaji wakati wa kusafirisha fedha.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment