Image
Image

SHIMIWI KUFANYA MKUTANO JUMAMOSI AGOSTI 31 KUJADILI MASHINDANO YA MWAKA HUU YATAKAVYO KUWA.


Kaimu Katibu wa Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) Bw.Moshi Makuka akisisitiza umuhimu wa vilabu kuzingatia sheria,kanuni na taratibu za mashindano ya SHIMIWI.

Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) linatarajia kufanya mkutano maalum wa kupanga ratiba ya mashindano ya SHIMIWI ya mwaka huu utakaofanyika kesho kutwa jumamosi ya agosti 31 majira ya saa 4 asubuhi katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora zilizopo mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu wa SHIMIWI Bw.Moshi Makuka alisema mkutano huo  utawahusisha wenyeviti na makatibu wa vilabu vya michezo ya SHIMIWI kutoka katika Wizara,Idara Zinazojitegemea,Sekretarieti za Mikoa na Wakala za Serikali.
“Wenyeviti na Makatibu wa Vilabu vinavyoshiriki michezo ya SHIMIWI mnatakiwa kuhudhuria mkutano huo bila kukosa ili kufanikisha mashindano ya SHIMIWI yatakayoanza hivi karibuni” alisema Bw.Makuka.
Bw.Makuka aliwataka wenyeviti na makatibu wa vilabu vyote kuja na viambatanisho muhimu kama vile barua za kuthibitisha kushiriki,fomu za usajili wa wachezaji watakaoshiriki na vikombe (kwa vilabu vilivyopata vikombe katika mashindano ya mwaka jana yaliyofanyika mjini Morogoro).
Mashindano ya michezo ya SHIMIWI kwa mwaka huu yamepangwa kufanyika mjini Dodoma kuanzia Septemba 21 hadi oktoba 5 ambapo yatahusisha michezo ya mpira wa miguu,netiboli,kuvuta kamba,riadha,baiskeli,karata,bao na drafti.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment