Mlango wa Katibu wa CCM wa tawi la Sinza E ukiwa umepigiliwa mbao kwa misumari kuzuia uongozi kuingia ndani.
Mlango wa Katibu wa CCM wa tawi la Sinza E ukiwa umepigiliwa mbao kwa misumari kuzuia uongozi kuingia ndani.
Sehemu ya kulaza magari inayolalamikiwa na vijana wa CCM tawini hapo.
Vijana wa CCM wakilinda geti ili viongozi wasiingie ofisini.…
VIONGOZI wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Tawi la Sinza E jijini Dar es Salaam wamefungiwa milango na
vijana wa chama hicho kwa madai kuwa kuna ubadhirifu wa fedha katika ofisi
hiyo.
Mwenyekiti wa Vijana wa
Tawi hilo, Ally Ngoti ameuambia mtandao huu kuwa tangu viongozi wao waingie
madarakani wamekuwa hawaelezi mapato ya ofisi hiyo yanakwenda wapi.
“Hapa tuna miradi mingi kama
vile egesho la magari ambalo linaingiza mamilioni ya fedha lakini hatuoni
zinakwenda wapi. Kuna fremu za maduka na watu wamepanga lakini fedha hatuzioni,
tumeamua kufunga milango ya ofisi ili wasiiingine mpaka kieleweke,” alisema
Ngoti na kudai kuwa viongozi hao hawawapendi vijana kwa kuwa wanawakosoa.
Hakuna kiongozi hata mmoja
aliyepatikana kujibu tuhuma hizo au kusema watafanya nini ili kufungua ofisi
yao.
(PICHA / HABARI: HARUNI SANCHAWA / GPL)
0 comments:
Post a Comment