Image
Image

INSTANBUL YAELEZWA KUWA MSTARI WA MBELE KUANDAA FAINALI YA MASHINDANO YA ULAYA 2020.




Shirikisho la soka nchini Uingereza linasema kuwa mji wa Instanbul upo katika mstari wa mbele kuandaa michuano ya nusu fainali na fainali ya mashindano ya barani Ulaya mwaka 2020.

Uingereza ilikuwa na matumaini ya kuandaa michuano hiyo katika uwanja wa Wembley lakini Katibu Mkuu wa FA Alex Horne anasema mji wa Istanbul unapigiwa kipaumbele baada ya kukosa nafasi ya kuandaa mashindano ya Olimpiki mwaka 2020.

Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA linasema kuwa michuano ya soka ya mwaka 2020 itaandaliwa katika miji 13 katika mataifa 32 ambayo yameomba kuandaa michuano hiyo, na uamuzi utatolewa mwezi Aprili mwaka ujao.

Awali, rais wa UEFA Michel Platini alisema kuwa angeunga mkono Uturuki kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ikiwa wangekosa nafasi ya kaundaa michuano ya Olimpiki mwaka 2020, baad aya Tokyo kupewa nafasi hiyo.

Mbali na Uturuki, Ukraine pia imeomba nafasi ya kuandaa michuano ya nusu fainali na fainali, huku mataifa mengine 25 ikiwemo Scotland wameomba nafasi ya kuandaa michuano ya makundi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment