Image
Image

KAMPUNI YA YA JAPANI KUUNDA BOMBA LA KUSAFIRISHIA MAFUTA KUTOKA SUDAN KUSINI.




Kampuni ya Toyota kutoka Japan ndiyo itakayo jenga bomba la kusafirishia mafuta kutoka Sudan Kusini hadi pwani ya Kenya. 

Hii ni kulingana na habari kutoka katika shirika la habari la Sudan Kusini na mradi huo utagharimu dola za kimarekani bilioni tano. 

Nchi ya Sudan Kusini itashirikiana na nchi za Kenya, Uganda na kampuni ya Toyota kuunda na kudumisha huduma za bomba hilo. 

Bomba hili litatoka nchini Sudan Kusini na kupitia Uganda na kisha kuingia Kenya hadi bandari ya Lamu na kutumika kusafirishia mafuta ya Sudan Kusini badala ya Kutumia Sudan. 

Pia kampuni hii itajenga bomba lingine kutoka magharibi mwa Uganda ili kutumika wakati Uganda itaanza uchimbaji wa mafuta yake baadaye mwaka wa 2017.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment