Image
Image

MASOGANGE NAWENZAKE WAPATA DHAMANA.AFRIKA KUSINI


Johannesburg. 

Watanzania Agness Masogange na Melisa Edward waliokamatwa kwa kutuhumiwa kubeba dawa za kulevya huko Afrika Kusini wameachiwa kwa dhamana.

Mkuu wa Kitengo cha Dawa za Kulevya Afrika Kusini, Kamishna Toto Mangaleni aliithibitishia Mwananchi jana kuwa watuhumiwa hao wameachiwa kwa dhamana,lakini wataendelea kubaki Afrika Kusini wakati kesi yao ikiendelea.

Mangaleni alisema wanawake hao ambao juzi pia walipanda kizimbani, walipata dhamana hiyo jana kutoka Mahakama Kuu ya Gauteng iliyoko eneo la Kempton Park jijini Johannesburg.

Hata hivyo, Kamishna Mangaleni alisema hawezi kuzungumzia zaidi kuhusu kesi hiyo kwa sababu hataki kuharibu uchunguzi ambao unaendelea dhidi ya Watanzania hao, ambao ni wasanii.

Marafiki wa karibu wa Masogange wanaoishi maeneo ya Midland Johannesburg ambao walikataa kunukuliwa majina yao, walithibitisha kuwa wanawake hao wameachiwa kwa dhamana.

“Ni kweli wameachiwa leo asubuhi. Lakini hatuwezi kuongelea kwa kina habari hizi kwa sababu hatutaki matatizo na polisi. Hii kesi bado inaendelea na wataendelea kubaki hapa hadi kesi yao itakapomalizika,” alisema mmoja wa marafiki zake.

Naye Masogange aliandika kwenye mtandao wa ‘Facebook’.
“Namshukuru Mungu nimeamini wewe ulikuwa pamoja na mimi katika maombi yangu na nashukuru kwa wote mliokuwa mkiniombea Mungu kapokea maombi yenu.”

Masogange na Melissa walikamatwa Julai 2 mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg wakiwa wana mabegi sita makubwa ya dawa zinazoaminika kuwa ni `Crystal Methyl Amphetamine’.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kuzuia na Kudhibiti Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa aliiambia Mwananchi jijini Dar es Salaam kuwa alikuwa amepata taarifa za kuachiwa kwa wasichana hao, lakini alikuwa anawasiliana na watu wa Afrika Kusini ili kupata uhakika.

Nzowa, hata hivyo alilidokeza gazeti hili juzi kuwa kuna uwezekano wanawake hao wangepata dhamana au kufungwa kifungo chepesi kwani dawa walizokamatwa nazo ni kemikali zinazotumika kutengeneza dawa za aina tofauti kwa matumizi ya binadamu ingawa pia na dawa za kulevya.
Mamlaka yapinga uamuzi wa Mahakama.

Msemaji wa Mamlaka za Huduma za Mapato Afrika Kusini(SARS), Marika Muller alisema wana uhakika asilimia 100 kuwa akina Masogange walikamatwa na dawa za kulevya.
“Timu yetu ilifanya kazi vizuri na ilitambua kuwa mzigo huo ulikuwa wa dawa za kulevya ila tunaiachia mahakama kuendelea na uchunguzi wake,” aliongeza Muller.

SOURCE: MWANANCHI
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment