Image
Image

RAIS KIKWETE AIHAKIKISHIA MAREKANI KUWA MASLAHI YA MAKAMPUNI YA MAREKANI YANAYOTAKA KUWEKEZA NCHINI HAYATAATHIRIWA NA KUWEPO KWA CHINA KATIKA UCHUMI WA TANZANIA.


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mabalozi wa heshima watakaoiwakilisha Tanzania katika majimbo mbalimbali nchini Marekani wakati wa hafla ya kuwapa hati za utambulisho zilizofanyika katika ubalozi wa Tanzania jijini Washington Marekani.

Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa maslahi ya makampuni ya Marekani yanayotaka kuwekeza katika Tanzania hayataathiriwa na kuwepo kwa China katika uchumi wa Tanzania kwa sababu China siyo moja ya wawekezaji wakuu katika uchumi wa Tanzania kwa sasa.

Amesema kuwa miongoni mwa wawekezaji wakuu wa uchumi wa Tanzania, China inashikilia nafasi ya 10 huku Uingereza ikiwa inaongoza katika kuwekeza katika Tanzania.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa China ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa misaada ya maendeleo kwa Tanzania lakini siyo katika makampuni ya nchi hiyo kuwekeza katika uchumi wa Tanzania na hivyo nchi hiyo haiwezi kuwa tishio kwa uwekezaji wa makampuni ya Marekani.

Ametoa ufafanuzi huo  wakati alipokutana katika mkutano wa kikazi na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Mahusiano ya Nje na Bajeti ya Miradi ya Maendeleo ya Bunge la Marekani mjini Washington, D.C., pamoja na baadhi ya wajumbe wa kamati yake.

Katika mkutano huo, Rais Kikwete aliulizwa jinsi gani fedha ya Jamhuri ya Watu wa China katika uchumi wa Tanzania inavyoathiri uwekezaji wa makampuni ya Marekani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment