Image
Image

TMU YA KIKAPU YA UFARANSA YAWEKA REKODI YA KUNYAKUWA KOMBE HUKO ULAYA.




Timu ya taifa ya kikapu nchini Ufaransa, imetwaa Kombe la mpira wa kikapo katika mashindano ya Ulaya ikiwa ni mara ya kwanza katika Historia ya mchezo huo.

Vijana wa Les Blues waliishinda Litunia kwa vikapo 80 kwa 66 ikiwa ni tofauti ya vikapo 14, ambapo wataalamu wa mchezo huu wanasema ni tafauti kubwa.

Wachezaji nyota waliotamba katika mchezo huo ni pamoja na Boris Diaw, Nicolas Batum pamoja na Tony Parker alieteuliwa kuwa mchezaji bora wa michuano hiyo ya mpira wa kikapo barani Ulaya.

Kulikuwepo na shaka upande wa Timu hiyo ya Ufransa, kwani walianza vibaya kwa kushindwa mara tatu katika mechi nane.

Lakini baadae vijana hao wa le Blues wamekamilisha kuwa  washindi wa michuano hiyo pale walipoanza kuinyuka Slovenia wenyeji wa michuano hiyo mbele ya mashabiki wake na baadae Uhispania bingwa mtetezi wa kombe hilo.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment