Image
Image

WANAUME WANNE WALOMBAKA MWANAMKE MMOJA NA KUMUUA WAHUKUMIWA KIFO HUKO INDIA.




Mahakama ya New Delhi, India imetoa hukumu ya kifo kwa wananume 4 waliombaka mwanamke mmoja na kisha kumuua Disemba mwaka uliopita. 

Jaji Yogesh Khanna akitoa hukumu hiyo amesema dhulma dhidi ya wanawake zimeshtadi mno katika miaka ya hivi karibuni nchini India na kwamba adhabu ya kifo inatolewa kwa washtakiwa ili iwe funzo kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Wanaume hao wanadaiwa kumbaka kwa zamu mwanamke mmoja kwenye basi na kisha kumtesa hadi kufa. Mshukiwa mwingine wa kesi hiyo alipatikana amejitia kitanzi gerezani. Kesi hiyo imekuwa ikiendeshwa kwa zaidi ya miezi saba na kufuatiliwa kwa karibu na vyombo vingi vya habari vya kimataifa.

Uchunguzi unaonyesha kuwa visa vya ubakaji na dhulma dhidi ya wanawake ni jambo la kawaida nchini India kutokana na utamaduni wao unaomsawiri mwanamke kama chombo tu cha kupambia dunia.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment