Image
Image

WANAWAKE NCHINI ZIMBABWE WAKASIRISHWA NA UAMUZI WA RAIS WA NCHI HIYO MUGABE WA KUTEUA WANAWAKE WA 3 KATIKA BARAZA LA MAWAZIR 26.




Makundi ya wanawake nchini Zimbabwe yamekasirishwa na uamuzi wa Rais Robert Mugabe wa kuteuwa wanawake watatu pekee katika baraza lake la mawaziri 2.

Akitetea uamuzi wake, Rais Mugabe amesema ni sharti wanawake wafanye vyema zaidi katika chaguzi ili waweze kupewa viti vya uwaziri. 

Wanawake nchini humo wanasema usawa wa kijinsia upo mbali sana kufikiwa. 

Inaelezwa kuwa ni asilimia 12 tu ya wanawake kwenye baraza la mawaziri ikilinganishwa na idadi ya wanawake nchini humo ambayo ni asilimia 52 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi iliyofanywa mwaka jana.

Baada ya kuwaapisha mawaziri Jumanne iliyopita, Rais Robert Mugabe aliwaambia waandishi habari kuwa, hakuna la kustaajabisha kwamba wanawake ni wachache kwenye baraza hilo.

 Alisema wanawake wanapaswa kupambana na wenzao wa kiume bila kutegemea kupendelewa kwa namna yoyote.

Katiba mpya ya Zimbabwe iliyoidhinishwa mapema mwaka huu inaelezea vipengele vya kisheria vinavyolinda wanawake ikiwemo kuwa na haki sawa katika ajira na uwakilishi sawa katika ofisi zote za umma, ambapo inategemewa kwamba usawa huo ni pamoja na uwakilishi kwenye baraza la mawaziri. 
Jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika SADC ambayo Zimbabwe ni mwanachama ina sheria inayosema wanawake wawe na uwakilishi wa kisiasa kwa asili mia 50 ifikapo mwaka wa 2015.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment