Image
Image

WATU KADHAA WAOKOLEWA KWENYE JENGO LA WESTGATE




Kamanda wa Polisi wa Nairobi ametangaza kukombolewa idadi ya watu kadhaa waliokuwa wakishikiliwa mateka na wanamgambo wa al Shabab ndani ya jumba la kibiashara la Westgate lililoko kwenye mtaa wa Westland jijini Nairobi nchini Kenya. 

David Kimaiyo amesema kuwa, kikosi cha usalama cha Kenya kimefanikiwa kutekeleza operesheni hiyo ya kuwaokoa baadhi ya watu waliokuwa wakishikiliwa na wanamgambo wa al Shabab na kusisitiza kwamba operesheni hiyo ya uokozi inaendelea kwa kasi kikubwa. 
Wakati huohuo, Polisi ya Kenya imeeleza kwamba inadhibiti ghorofa zote za jengo la kituo hicho cha biashara. 
 
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, baada ya masaa machache itafanyika operesheni ya kumaliza kabisa tukio hilo lililodumu kwa siku tatu. Hadi sasa inaelezwa kuwa, watu wasiopungua 69 wameuawa na wengine wasiopungua 200 kujeruhiwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment