Image
Image

UKOSEFU WA ELIMU YA NIDHAMU YA MATUMIZI YA FEDHA, WAAJIRI WASHAURIWA KUTOA MAFUNZO KWA WASTAAFU WATARAJIWA.


Hawa Ghasia - Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa.

Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa Hawa Ghasia amesema ukosefu wa elimu ya  nidhamu ya matumizi ya fedha kwa wastaafu  nchini kunachangia kwa kiasi kikubwa kuwa na maisha duni mara baada ya kulipwa mafao yao kwa mkupuo.

Akifungua mkutano wa 6 wa mwaka wa wadau wa mfuko wa pensheni wa LAPF waziri ghasia amesema waajiri wengi nchini bado hawajawa na utaratibu wa kutoa mafunzo kwa wastaafu watarajiwa pale muda unapofika hali ambayo imekuwa ikichangia kushindwa kutumia vyema mafao yao.

Kwa upande wake waziri wa kazi na ajira Gaudensia Kabaka amesema mifuko ya hifadhi ya jamii na waajiri nchini bado wanakazi kubwa ya kuelimisha jamii umuhimu wa kuchangia kwenye mifuko hiyo ili waondokane  na  dhana kuwa mifuko hiyo ni kwajili ya watumishi wa serikali na watu matajiri tu.

Mkutano huo wa siku mbili unawashirikisha wadau mbalimbali wa mfuko huo zaidi ya mia tano kutoka ndani na nje ya nchi ambapo mada mbalimbali zitajadiliwa na kaulimbiu ya mkutano huo mwaka huu ni kukidhi kwa mafao ya kustaafu changamoto na njia za kuboresha.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment