Image
Image

SERIKALI YASEMA BADO INATAFAKARI KWAKINA JUU YA UWEZEKANO WA KUMRUDISHA MTOTO WAKIKE SHULENI ALIYE KATISHA MASOMO KWA SABABU ZA KUBEBA UJAUZITO,


Baadhi ya wanafunzi  shule ya jkt wakionekana wakisikiliza jambo kwa umakini mkubwa juu ya siku ya maadhimisho ya  mtoto wa kike (Picha na Maktaba Yetu).

Serikali imesema bado inaangalia uwezekano wa kuweka utaratibu wa kumrudisha shuleni mtoto wa kike aliyekatisha masomo baada ya kupata ujauzito.

Hatua hiyo inafuatiwa kubainika kwamba idadi kubwa ya watoto wa kike wanaopata ujauzito hawafanyi hivyo kwa kupenda bali kwa kulazimishwa ama kurubuniwa na wanaume wakatili .
 Baadhi ya wanafunzi wakionekana kujadili jambo(Picha na Maktaba Yetu).
Hali hiyo imebainishwa na Mkurugenzi wa masuala Mtambuka katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk. Leticia Sayi wakati akizungumza katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mtoto wa kike, jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo amewataka wadau wa masuala mbalimbali wakiwemo wa elimu kuungana na serikali kuhakikisha vitendo vyote vya unyanyasaji dhidi ya mtoto wa kike vinakomeshwa kwani vimekuwa na athari kubwa kimwili, kisaikolojia na kiuchumi.
Baadhi ya wasichana wakiwa wanajadiliana jambo(Picha na Maktaba Yetu).
Maadhimisho ya siku ya kimataifa ta Mtoto wa Kike kwa Tanzania yameratibiwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo WILDAF Tawi la Tanzania kwa kushirikiana na Mtandao wa Wanawake Waelimishaji Afrika FAWE yakiwa na kauli mbiu ya Ubunifu kwa ajili ya Elimu ya Wasichana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment