Image
Image

MELI YENYE UREFU WA MITA 250 YATIA NANGA KATIKA BANDARI YA DAR ES SALAAM,HUKU IKIWA NA UREFU WA KUBEBA KONTENA ZIPATAZO 4,500.


 Hii Ndio meli yenye urefu wa Mita 250 ikionekana ikiwa imebeba makontena Baada ya kutia nanga hii leo katika Gati la Bandari ya Dar es Salaam.

Na. Salum Mkambala,DSM.
Tanzania kwa mara ya kwanza imepokea meli kubwa yenye urefu wa mita 250 sawa na uwanja wa mpira wa miguu miwili na nusu ambayo inauwezo wa kubeba kontena elfu nne na mia tano zenye futi ishirini elfu ikiwa ni siku moja tu tangu serikali irudishe utaratibu wa awali kwa kipindi cha mwezi mmoja wa kupitisha malori katika mizani hapa nchini.
Hii Ndio meli yenye urefu wa Mita 250 ikionekana ikiwa imebeba makontena Baada ya kutia nanga hii leo katika Gati la Bandari ya Dar es Salaam, Huku baadhi ya watu wakiitizama kwa ukaribu kufuatia ukubwa iliyo nao.
Akishuhudia meli hiyo iliyopewa jina la MAERSK CUBANGO ikitia nanga katika gati ya bandari ya DSM waziri wa uchukuzi Dkt,HARRISON MWAKYEMBE ameeleza kuwa Tanzania haijawahi kupokea meli kubwa kama hiyo na mara nyingi meli tulizozea ni za kubeba kontena 2000 tu na meli kama hizo huwa zinaishia katika Bandari ya Mombasa nchini Kenya.
Aidha Dkt,MWAKYEMBE ametumia nafasi hiyo kuwatolea wito taasisi za mabenki na TRA pamoja zingine mtambuka katika shuguli za kupakua na kupakia mizigo bandarini  kukesha katika bandari ili kupunguza mizigo katika bandari hiyo ambapo amesema kwa sasa katika kipindi cha muda kadhaa bandari hiyo itakuwa ikifanya kazi kwa saa 24.
Waziri wa Uchukuzi nchini DK. Harrison Mwakyembe, Akizungumza na waandishi wa habari juu ya ujio wa meli hiyo yenye urefu wa Mita 250, ambayo inaonekana ikiwa imebeba makontena Baada ya kutia nanga katika Gati la Bandari ya Dar es Salaam, Huku baadhi ya watu wakionekana kumsikiliza waziri huyo akizungumza kwa umakini.
Hii Ndio meli yenye urefu wa Mita 250 ikionekana ikiwa imebeba makontena Baada ya kutia nanga hii leo katika Gati la Bandari ya Dar es Salaam.
Akizungumza mbele ya waziri huyo kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya bandari NCHINI,TPA.mhandisi,MADENI KIPANDE ameeleza mgomo wa siku nne wa wamiliki wa malori umeiletea hasara ya sh.bilion 1.5 bandari hiyo ambapo meli 18 zilikwama nje ya bandari na meli tisa zilikwama katika GATI ya bandari ambapo meli hiyo imeletwa kwa majaribio kwa ushirikiano wa wakala wa meli ya MAERSK na mamlaka hiyo baada ya kufanya utafiti wa kina ambapo nahodha mtanzania Abdul Mwingamno alifanikiwa vyema kuegesha meli hiyo katika gati.
Wakati huo huo wakiwawakilisha wafanyabiashara wenzao wa malori mfanyabiashara AZIM DEWJI na KARIM LADHA wamedai licha ya serikali kumaliza mgomo kusubiri kamati kutoa majawabu lakini magari yanazuiwa kupita katika mizani ambapo wanatarajia kuifikisha wizara ya ujenzi mahakamani baada ya kufanya tathmini ya hasara waliyoipata. 
Haya ni malori yakiwa yanaonekana na nyuma yakionekana makontena.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment