Katibu Mkuu Wizara ya fedha Dkt. Silvacius Likwelile
aliyesimama akisalimia ujumbe wa Tanzania pamoja na baadhi ya watanzania
waishio Marekani kabla ya kuanza kwa hafla ya chakula cha jioni ubalozi wa
Tanzania – Marekani.
Balozi wa Tanzania Marekani na Mexico Mhe. Liberata
Mulamula akitoa utambulisho wa viongozi wakati wa chakula cha jioni kwa ujumbe
wa Tanzania na baadhi ya watanzania waishio Marekani.
Waziri wa Fedha Dkt. Wiliam Mgimwa akiongea machache
wakati wa chakula cha jioni katika ubalozi wa Tanzania nchini Marekani kulia
kwake ni Balozi wa Tanzania Marekani na Mexico Mhe. Liberata Mulamula.
Kutoka kulia Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano
Dkt. Wiliam Mgimwa, Waziri wa Fedha Zanzibar Bw. Yusuph Mzee, Naibu Gavana wa
BOT Dkt. Natu Mwamba wakati wa chakula cha pamoja.
Kutoka kulia wachumi Wizara ya Fedha Bw. Pima Patrick na
Erasto Kivuyo wakijipatia chakula cha jioni.
Picha zote na Bi. Ingiahedi Mduma na Bi Eva Valerian –
Washington DC
0 comments:
Post a Comment