Image
Image

KENYA YAAHIDI KUSHIKAMANA NA TANZANIA ILI KUHAKIKISHA INAIMARISHA NGUZO YA AFRIKA MASHARIKI


                                  Amina Mohammed


Waziri wa Mambo ya Nje wa  Kenya, Amina Mohammed amesema nchi yake itaendelea kushikamana na Tanzania katika kujenga Jumuiya imara ya Afrika Mashariki.

Akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Waziri Amina Mohammed ameisifu hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa bungeni Dodoma hivi karibuni na kupongeza msimamo wa Tanzania wa kutojitoa katika Jumuiya hiyo.

Amesema Tanzania na Kenya ni nchi waanzilishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na amesisitiza kwamba haiwezekani kujenga Afrika Mashariki madhubuti kwa kuitenga Tanzania.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje wa Kenya aliwasili nchini jana jioni ambapo amekuwa na mazungumzo ya faragha na mwenzake wa Tanzania, Bernard Membe katika masuala ya Mustakabali wa Afrika Mashariki, Uhusiano wa Tanzania na Kenya na Kesi za ICC.

Hivi karibuni, nchi tatu wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda, Kenya na Rwanda zimekuwa zikifanya mambo ambayo yameonekana kuzibagua Tanzania na Burundi kiasi cha kuibua sintofahamu juu ya mustakabali ya Afrika mashariki pamoja na hofu kuhusu utengamano wa jumuiya hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment