Image
Image

DRC yahimizwa ikubali msaada wa MONUSCO

Umoja wa Afrika (AU) umeitaka serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikubali kusaidiwa na vikosi vya Umoja wa Mataifa katika kupambana na waasi wa mashariki mwa nchi hiyo, baada ya mzozo juu ya tuhuma za ukiukaji wa haki za binadamu dhidi ya majenerali wa jeshi la Kongo kuvuruga mpango wa operesheni za pamoja dhidi ya waasi hao.
Vikosi vya Umoja wa Mataifa vya kulinda amani nchini Kongo DR vya MONUSCO vilikuwa vitoe msaada kwa jeshi la Kongo katika operesheni ya kupambana na waasi wa FDLR, lakini operesheni hiyo ilisimamishwa mwezi huu baada ya majenerali wawili wa jeshi la Kongo waliokuwa waongoze operesheni hiyo kutuhumiwa kuhusika na ukiukaji wa haki za binadamu. Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alisema wiki iliyopita kwamba operesheni hiyo ilikuwa imeshaanza bila ya msaada wa vikosi vya MONUSCO. 
Baada ya kikao cha wajumbe wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika kilichofanyika hapo jana, mwakilishi maalumu wa AU katika eneo la Maziwa Makuu Boubacar Gaoussou Diarra, alivieleza vyombo vya habari kuwa umoja huo unahisi kuna haja ya kufanyika operesheni ya pamoja ili kuweza kupata mafanikio na kwamba haujafurahishwa na uamuzi wa serikali ya Kinshasa wa kukataa misaada ya kilojistiki na kitaalamu ya MONUSCO
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment