Image
Image

Waandishi wahabari watakiwa kutumia kalamu zao kuandika habari za kweli kuliko kupotosha Umma

Jeshi la polisi mkoa wa TANGA limetoa wito kwa wanahabari kuacha kutoa taarifa zisizo sahihi kuhusu swala la majambazi waliokua wamejificha kwenye pango lililo jirani na mapango ya utalii ya amboni,wiki moja iliopita.
Kamanda wa Polisi mkoa wa TANGA, FRAISHER KASHAI ametoa wito huo katika kikao chake na waandishi wa habari. Mwandishi wetu BERTHA MWAMBELA alihudhuria mkutano huo na hii ni taarifa yake.
Akizungumza na wanahabari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Fraisher Kashai amesema wapo baadhi ya wanahabari wanatoa taarifa zisizo sahihi jambo linalosababisha hofu kwa wakazi wa Tanga,na hata wageni wanaokuja kufanya shughuli za utalii katika mapango ya amboni.
Jambo jingine lililozungumzwa na kamanda Kashai ni namna walivyojipanga kudhibiti hali ya wageni wanaoingia kwenye makazi ya watu bila taarifa kuanzia ngazi ya kata.
Hata hivyo jeshi la polisi linawashikilia watu kadhaa kutokana na uporaji wa silaha kwa askari polisi wawili waliokua doria tarehe 26 mwezi wa kwanza mwaka huu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment