Na.Msaka Noti
Wachimbaji watatu wadogo wa madini ya dhahabu wamekutwa wamekufa
kwenye shimo la Urefu wa Futi 50 walikokuwa wakichimba dhahabu baada ya
kuangukiwa na Kifusi katika kitongoji cha Mawowo, kijiji cha Patamela, kata ya
saza,tarafa ya kwimba,wilaya ya chunya, Mkoa wa Mbeya.
Kwamujibu wa kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya SACP-
Ahmed Msangi amesema kuwa chanzo cha tukio hilo la kupoteza maisha kwa
wachimbaji hao wadogo wa madini katika shimo hilo nikutokana na kuta za shimo
hilo kulowa maji na hivyo kukosa uimara na kiasha kuporomoka na kusababisha
vifo.
Aidha Kamanda Msangi amewataja waliopoteza Maisha baada ya
kuwatambua kuwa ni wanaume ambao umri wao nikuanzia miaka 26 hadi 35 ambapo
mmoja kati ya hao watatu ni Victor Sanga ni Mkazi wa Mbeya ila wawili walio baki
hawakutambuliwa maramoja kuwa niwakazi wawapi na kwamba miili yao imehifadhiwa kwenye hospitali ya Mwambani
Chunya, Hivyo Upelelezi zaidi wa tukio hilo unaendelea.
·
WATU WATATU WAFARIKI DUNIA BAADA YA
KUANGUKIWA NA KIFUSI WAKIWA KATIKA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MADINI.
·
MTU MMOJA AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI
YA BARABARANI JIJINI MBEYA.
·
WATU WAWILI WANASHIKILIWA NA JESHI
LA POLISI MKOA WA MBEYA WAKIWA NA KETE ZA BHANGI.
·
KATIKA TUKIO LA KWANZA:
·
WATU WATATU WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA
YA 1. VICTOR SANGA (26) MKAZI
WA MBEYA 2. AMEFAHAMIKA KWA JINA
MOJA LA SHETA UMRI KATI YA MIAKA
30-35 NA 3. HAJAFAHAMIKA JINA WALA
MAKAZI, JINSI YA KIUME, UMRI KATI YA MIAKA 30-35, WOTE WACHIMBAJI WADOGOWADOGO
WA MADINI/DHAHABU WALIKUTWA WAMEKUFA
KWENYE SHIMO LENYE UREFU WA FUTI 50 WALIMOKUWA WAKICHIMBA DHAHABU BAADA YA KUANGUKIWA
NA KIFUSI.
·
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 11.03.2015 MAJIRA YA SAA 19:15 JIONI HUKO KATIKA KITONGOJI
CHA MAWOWO, KIJIJI CHA PATAMELA, KATA YA SAZA, TARAFA YA KWIMBA, WILAYA YA
CHUNYA, MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA CHANZO TUKIO HILO NI BAADA YA KUTA ZA
SHIMO KULOA MAJI NA KUKOSA UIMARA NA KISHA KUPOROMOKA.
·
MIILI YA MAREHEMU IMEHIFADHIWA
HOSPITALI YA MWAMBANI CHUNYA. UPELELEZI ZAIDI WA TUKIO HILI UNAENDELEA.
·
KATIKA TUKIO LA PILI:
·
MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA STEWARD MANDRAS (55) MKAZI WA UYOLE ALIFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA
GARI LISILOFAHAMIKA LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA ASIYEFAHAMIKA.
·
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 11.03.2015 MAJIRA YA SAA 19:10 JIONI HUKO ENEO LA
SIJABAJE-UYOLE, KATA YA IGAWILO, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA HOSPITALI YA
RUFAA MBEYA. DEREVA ALIKIMBIA NA GARI MARA BAADA YA TUKIO, JITIHADA ZA
KUMTAFUTA ZINAENDELEA.
·
TAARIFA ZA MISAKO:
·
WATU WAWILI WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA
YA 1. DIAMUND MANYERERE (24) MKAZI WA MOPOROMOKO NA 2. REMSI BUNGE (20) MKAZI WA MAKAMBINI
WILAYANI MOMBA WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA WAKIWA NA BHANGI KETE 03 SAWA NA UZITO WA GRAM 15.
·
WATUHUMIWA WALIKAMATWA KATIKA MSAKO
ULIOFANYIKA MNAMO TAREHE 11.03.2015
MAJIRA YA SAA 08:00 ASUBUHI HUKO
KATIKA MSITU WA IDARA YA MAJI, KATA NA TARAFA YA TUNDUMA, WILAYA YA MOMBA, MKOA
WA MBEYA. TARATIBU ZA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.
·
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA
MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z.
MSANGI ANATOA WITO KWA WACHIMBAJI MADINI KUWA MAKINI HASA KATIKA KIPINDI
HIKI CHA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA KWA KUCHUKUA TAHADHARI ILI KUEPUKA MADHARA
YANAYOWEZA KUEPUKIKA. AIDHA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI
ALIPO DEREVA ALIYESABABISHA KIFO NA KISHA KUKIMBIA AZITOE ILI AKAMATWE NA HATUA
ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAKE.
·
Imesainiwa na:
·
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
·
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
0 comments:
Post a Comment