Mjumbe wa Umoja wa
Afrika nchini Somalia Maman Sidikou amesema askari hao watatu walishambuliwa
ghafla katika eneo la Lower Shabelle huko kusini mwa Somalia.
Hata hivyo msemaji
wa kundi la al Shabab Abdulaziz Abu Musab amesema kundi hilo limeua askari 5 wa
Umoja wa Afrika na kwamba wote walikuwa kutoka Burundi. Umoja wa Afrika
haukueleza utambulisho wa askari hao.
Siku moja kabla ya
mauaji hayo wapiganaji wa kundi la kigaidi la al Shabab pia walikuwa wameua
askari watatu wa Kenya wanaohudumu katika kikosi cha majeshi ya Afrika
yanayolinda amani nchini Somalia AMISOM na kujeruhi wengine 8.
0 comments:
Post a Comment