Image
Image

Dk.Shein:Matibabu ya Bongo na Uti wa mgongo ni hatua muhimu ya kuimarisha huduma za afya Zanzibar.



Rais  wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dr.Ali Mohmaed Shein amesema ahadi alizozitoa  za afya  asilimia kubwa zimetekelezwa ikiwemo ya kitengo cha matibabu ya ubongo na uti wa mgongo.

Dr. Shein ametoa kauli hiyo ikulu wakati alipokutana na madakatari bingwa wa kichwa  na  uti wa mgongo na Afrika mashariki ambao walifika ikulu kuonana naye,ambapo Dr Shein amemsmea kati ya ahadi tatu aliozoziahidi wkati akifungua baraza la wawakilishi mwaka 2010 mara baada ya kuunda serikali aliahidi  kuanizsha huduma tatu ambazo  ni upasuaji wa Moyo,matibabu ya njia za chakula na maradhi ya njia za mkojo  na figo  ambapo ni huduma ya upasiaji wa moyo pekee ndiyo  mandalizi hayajakamilika huku akifurahishwa na hatua za kitengo cha kichwa  na uti wamgongo  kuwa ni moja ya kituo kikubwa  afrika mashariki.


Kwa upande wake Daktari bingwa wa upasuaji mishipa Dr.Mahmuod Qureshi amesema taasisi hiyo ya Zanzibar  ni muhimu sana na ndio maana wataalamu  wengi wamekuja kujifunza hapo.

Kwa upande wake  mkurugenzi mkuu wa hospitali ya mnazi mmoja Dr. Jamala Adam Taibu amesema tayari kituo hicho kimeshafanya upauaji wa wagonjwa 713 wakiwemo watoto 212 waliofanyiwa upauaji wa vichwa na 78  uapasuaji wa uti wa mgongo,huku wengine 62-ubongo,uapsuaji wa uti 183 hukuwengine wakifanyiwa upauaji wa kuondoa uvimbe wa mafuta na Saratani ya damu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment