Image
Image

News Alert: Makundi ya wazee yapaza sauti zao kwa serikali kuhakikisha inakemea hospitali zake kwa kushindwa kuwa tambua na kupinga sera zao.


Makundi ya wazee walio na zaidi ya umri wa miaka 60 na kuendelea wameiomba serikali kuingilia kati kufuatia hospitali zake kuipinga sera hiyo kwa madai kuwa hawaitambui hatua inayosababisha sehemu kubwa ya makundi hayo kuathirika na wengine kupoteza maisha kwa kukosa huduma.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mazinde wilayani Korogwe na kuhudhuriwa na wadau wa afya ngazi ya wilaya,viongozi wa serikali na kamati ya ulinzi na usalama chini ya Mwenyekiti wake mkuu wa wilaya hiyo wazee hao wamesema mbali na sera hiyo kupingwa,pia kadi zao za uanachama wa mfuko wa afya ya jamii (CHF) zinashindwa kutambuliwa wanapokwenda kupata huduma katika kituo cha afya cha mombo na hospitali ya wilaya ya korogwe.

Hata hivyo mwenyekiti wa bodi ya afya wa wilaya ya korgwe Bwana Charles Gawile amewataka wananchi wa eneo hilo kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa kwa viongozi wa bodi hiyo endapo kuna hujuma za ubathirifu wa dawa zinazopelekwa katika zahanati ya kata yao zinazosimaiwa na kamati ya afya ngazi za vijiji ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Kufuatia hatua hiyo daktari wa zahanati ya kata ya Mazinde ambayo imesajiliwa na mfuko wa afya ya jamii Dr,Dunstan Wandi amesema malalamiko ya wananchi kuwa hawapati dawa hayasababishwi na viongozi wa afya na badala yake unapoagiza dawa bohari kuu ya dawa nchini (MSD) wanatekeleza baada ya miezi minne hatua ambayo imesababisha kero na wananchi kukataa kujiunga na mfuko huo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment