Image
Image

Serikali wilayani Ngorongoro mkoani Arusha imezionya baadhi ya taasisi zisizo za kiserikali zinazosababisha uvunjifu wa amani katika eneo la Ngorongoro.


Serikali wilayani Ngorongoro mkoani Arusha imezionya baadhi ya taasisi zisizo za kiserikali na baadhi ya viongozi ambao wanadaiwa kuchochea migogoro ndani ya jamii na kuwatetea baadhi ya wageni wanaoingia nchini kinyume cha sheria wakiwa na makundi ya mifugo hali ambayo inasababisha uvunjifu wa amani katika eneo la Ngorongoro.

Akiongea na viongozi wa kimila na baadhi ya viongozi wa serikali wakiwemo madiwani wa halmashauri ya wilaya ya ngorongoro, mkuu wa wilaya ya Ngorongoro,Hashim Mghandiwa amesema wilaya ya Ngorongoro imekuwa na sifa mbaya kitaifa na kimataifa kutokana na changamoto hizo ambazo zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi ili eneo hilo liendelee kuwa na amani na ameonya kuwa kiongozi yeyote atakayesababisha uvunjifu wa amani atakamatwa na pia ameahidi kuchukua hatua kali dhidi ya taasisi zisizo za kiserikali ambazo zinakwenda kinyume na katiba zao.

Nao baadhi ya viongozi wa kimila wa tarafa ya Ngorongoro akiwemo mwenyekiti wa baraza la wafugaji Metui Ole Shaudo wamekiri kuwepo kwa migogoro ambayo imechangia kuvuruga amani lakini pia wamewalaumu baadhi ya wawekezaji ambao nao wamekuwa kichocheo cha migogoro kwa wananchi kutokana na kupanua maeneo na baadhi kuyatumia kinyume na malengo yaliyomo kwenye mikataba yao.

Katikia mkutano huo baadhi ya viongozi wa kimilia wameiomba serikali kuwashirikisha kikamilifu viongozi wa jamii kwani wanajua matatizo mengi na mbinu za kuyatatua kama njia muhimu ya kuimarisha ulizi na usalama wa wananchi wa wilaya hiyo ya Ngorongoro.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment