Image
Image

News Alert: Watu wasiojulikana wafanya hujuma kubwa ya nguzo za umeme Arumeru


Watu wasiojulikana wakiwa na silaha za jadi zikiwemo mashoka,mapanga na misumeno wamefanya uharibifu mkubwa wa kukata na  kuangusha nguzo za umeme katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya arumeru tukio ambalo licha ya kulisababishia shirika hasara  kubwa lingeweza kusababisha maafa makubwa kwa wananchi.
Meneja wa Tanesco mkoa wa Arusha Bw.Jenesisi  Kakore amesema hujuma hizo zilizofanywa  usiku zimesababisha sehemu kubwa ya nyaya zilizokuwa na moto kuanguka chini jambo ambalo  ni hatari kubwa kwa maisha ya watu na viumbe wengine.
Aidha Bw.Kakore amewata wananchi kuona umhimu wa kulinda miundombinu ya umeme na  kutokubali kufumbia macho uharibifu kama huo kwani watu hao licha ya kuwacheleweshea  kufikiwa na huduma wanachezea kodi zao.
Viongozi na wananchi wa vijiji vya  kata ya orkokola ilikofanyika hujuma hiyo  wamesema  huenda iefanywa na watu wenye chuki ambao maeneo yao bado  hayafikiwa na huduma hiyo.
Hata hivyo Bw. Kakore amewaomba wananchi wenye malalamiko na kero mbalimbali   kuzifikisha ofisini kwake na kuachana na dhana potofu ya kufanya hujuma kwani licha ya  kuwa kinyume cha sheria  sio suluhisho la tatizo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment