Kiongozi
mkuu wa chama cha ACT wazalendo ndugu Zitto Zuberi Kabwe ameitaka serekali
kuhakikisha inawabana wamiliki wa mabasi kote nchini ili kuweza kutoa mikataba ya kazi
kwa madereva wao ili waweze kujulikana, kwa kufanya hivyo kuta
punguza ajali ambazo siyo za msingi.
Kauli
hiyo ameito wakati alipokuwa akiwahutubia mamia ya wakazi wa manispaa ya Singida
na viunga vyake kwenye mkutano wa kunadi chama cha ACT.
Kiongozi
mkuu wa chama hicho Bwana. Zitto Kabwe ,amesema kuwa aliyekuwa waziri wa uchukuzi Dk Harsson Mwakyembe
aliunda tume ya uchunguzi wa ajali na mpaka sasa majibu hayaja tolewa jambo
ambalo limekuwa likisababisha ajali kuendelea kutokea na kwa kipindi cha mwenzi
Mach na April mwaka huu zaidi wa watu mianane wamesha poteza maisha kutokana na
ajali za barabarani.
Ndugu Zitto
amesema kuwa ilikupunguza ajali hizi za barabarani ambazo zimekuwa zikitokea
kila uchao na kugharimu maisha ya watanzania wasio na hatia na kuwaacha na
ulemavu na wengine kupoteza maisha chama hicho cha ACT kimeitaka serikali kutoa
taarifa ya tume ya uchunguzi wa ajali za barabarani zilizo fanyiwa utafiti
ili kuweza kutafuta namna yakutatua matatizo ya ajali za mara kwa mara
zinazotokea nchini.
Kwaupande
mwingine mwenye kiti wa chama cha ACT Bi. Anna Mghwira na kada wa chama hicho
Bwana Selemani Msindi maarufu kwa jina la (Afande Sele) wamesema huduma
nyingi hasa za afya wakati wa zamani zilikuwa zikipatikana kulingana na
uwezo wa serikali wakati ule, na kwasasa nchi imekuwa na utajiri mwingi wa
madini ,kilimo na biashara,lakini cha kushangaza fursa hizo zimekuwa zikitumiwa
na baadhi ya watu.
0 comments:
Post a Comment