Image
Image

Lubuva amewahakikishia watanzania kuwa uchaguzi utafanyika tarehe iliyo pangwa.


Wakati makundi mbalimbali yakilalamikia kusuasua kwa zoezi la uandikishaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia mashine  BVR na kuzua hofu ya kuathiri uchaguzi mkuu ujao mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi jaji Damian Lubuva amewahakikishia watanzania kuwa uchaguzi utafanyika tarehe iliyo pangwa huku tume hiyo ikiongeza mashine 1550 ili kuchochea kasi ya uandikishaji.
Mwenyekiti huyo wa NEC ametoa  kauli hiyo katika ziara ya kukagua uandikishaji wa daftari hilo mkoani Dodoma ambapo akiwa wilayani Chemba anakanusha madai kuwa zoezi hilo linasuasua na kuwataka wananchi katika mikoa ambayo haijafikiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha.
Wakati jaji Lubuva akitoa kauli hiyo wakazi wa baadhi ya maeneo yaliyopitiwa na zoezi hilo la uandikishaji bado wanaendelea kulalamikia uendeshaji wake ambapo inawalazimu kutumia mpaka siku tatu kwenye foleni bila mafanikio huku wakihofu kukosa haki yao ya kikatiba ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu ujao.
Kwa upande wao baadhi viongozi wa siasa ambao wamekuwa wakitoa hamasa kwa wananchi kujiandikisha wameiomba serikali kuongeza muda wa uadikishaji hasa kwenye maeneo ambayo yana idadi kubwa ya watu ili kila mwenye sifa za kujiandikisha apate haki hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment