Image
Image

EAC yapokea taarifa ya nanma gani watatatua mgogoro nchini Burundi.


Siku moja kabla Marais wa jumuia ya Afrika Mashariki kukutana jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujadili Mgogoro wa Burundi, mawaziri wa mambo ya nje wa jumuia hiyo wamepokea taarifa ya mwenyekiti wa mawaziri wa jumuia hiyo pamoja na washauri maalum wa mzozo huo.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh.Bernad Membe amesema kutokana na jaribio la mapinduzi lililofanyika nchini burundi hivi karibuni kikao kilichopita kiliamua wakutane tena ili kujadili suala hilo.
Aidha amesema mbali na kupokea taarifa hizo wanasheria wakuu wa afrika mashariki watatoa taarifa kuhusu uamuzi wa mahakama ya katiba ya burundi juu ya rais pierre nkurunziza kugombea kwa mara ya tatu na baada ya kuunganisha taarifa zote hizo ndipo wataziwasilisha kwa marais hao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment